NYOTA wa Bayern Munich, Robert Lewandowski jana amekabidhiwa tuzo ya Kiatu cha Dhahabu Ulaya 2021 baada ya kuwa mfungaji bora wa bara hilo msimu uliopita 2020/21.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Poland, Lewandowski alifunga mabao 41 katika mechi 29 za Bundesliga akifuatiwa na Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.
Wakati Muargentina, Messi alifunga mabao 30 akiwa Barcelona kwenye La Liga, Mreno Cristiano Ronaldo alifunga mabao 29 akiwa Juventus katika Serie A.
0 comments:
Post a Comment