TIMU ya Liverpool imeibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya wenyeji, Leeds United usiku wa Jumapili katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Elland Road.
Mabao ya Liverpool yamefungwa na Mohamed Salah dakika ya 20, hilo likiwa bao lake la 100 katika Ligi Kuu ya England, Fabinho dakika ya 50 na Sadio Mane dakika ya 90 na ushei, huku Leeds ikimaliza pungufu baada ya Pascal Struijk kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja moja dakika ya 60 kwa kumchezea rafu Harvey Elliot kufuatia kuingia dakika ya 33 kuchukua nafasi ya Diego Llorente.
Kwa ushindi huo, Liverpool inafikisha pointi 10 sawa na Manchester United na Chelsea baada ya wote kucheza mechi nne sasa wakifuatana nafasi tatu za juu, wakati Leeds inabaki na pointi zake mbili za mechi nne pia katika nafasi ya 17 kwenye ligi ya timu 20.
Mikel Arteta makes Arsenal vow before title showdown at Man City, Eddie
Howe has the 'fire' to carry on at Newcastle... and Andoni Iraola opens up
on his Bournemouth exit: PREMIER LEAGUE LIVE
-
As we get to the business end of the Premier League season, all 20 clubs
are in action over the next three days and a host of managers are talking
today. K...
3 hours ago


.png)
0 comments:
Post a Comment