UONGOZI wa Simba SC umetoa kiasi cha fedha, Sh Milioni 10 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala kwa ajili ya kusaidia afya ya mama na mtoto kuelekea tamasha la Simba Day Jumapili Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Siku hiyo Wekundu hao wa Msimbazi watamenyana na mabingwa mara nne Afrika, TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) baada ya kutambulisha kikosi chao kizima cha msimu mpya.
0 comments:
Post a Comment