TIMU ya Namungo imeendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuwachapa wenyeji, Yosso Boys 2-0 katika mchezo wa Kundi A jioni ya leo Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Mabao ya Namungo FC yamefungwa na Sixtus Sabilo dakika ya 53 na Relliant Lusajo dakika ya 90 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi sita kufuatia kuilaza Meli 4 City katika mchezo wa kwanza Jumapili.
0 comments:
Post a Comment