SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limetaja tarehe za michezo wa Hatua ya 32 Bora ya Kombe la shirikisho hilo, maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC).
Katika ratiba hiyo, Azam FC watakuwa wenyeji wa Transt Camp Januari 28 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, wakati Yanga watamenyana na Mbao FC Januari 29 na mabingwa watetezi, Simba watacheza na Dar City Januari 30, mechi zote hizo mbili zikipigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment