• HABARI MPYA

    Monday, January 10, 2022

    LIVERPOOL YASONGA MBELE KIBABE KOMBE LA FA ENGLAND


    TIMU ya Liverpool imetoka nyuma na kushinda 4-1 dhidi ya Shrewsbury Town katika mchezo wa Raundi ya Tatu Kombe la FA England usiku wa Jumapili Uwanja wa Anfield.
    Daniel Udoh alianza kuwafungia wageni dakika ya 27, kabla ya Liverpool ‘kuliamsha dude’ kwa mabao ya Kaide Gordon dakika ya 34, Fabinho mawili, moja kwa penalti dakika ya 44 na lingine dakika ya 90 na ushei na Roberto Firmino dakika ya 78.
    Mechi nyingine, Tottenham pia imetoka nyuma na kuichapa Morecambe 3-1 wakati West Ham imeitoa Leeds United.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YASONGA MBELE KIBABE KOMBE LA FA ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top