KLABU ya Azam FC imembadilishia rasmi majukumu Abdi Hamid Moallin, Mmarekani mwenye asili ya Somalia kutoka Mkurugenzi wa Ufundi wa Maendeleo ya Soka la Vijana hadi Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza.
Moallin amekuwa kaimu kocha wa kikosi cha kwanza kwa takriban mwezi sasa tangu kuondolewa kwa kocha Mzambia, George Lwandamina na baada ya kazi yake nzuri amepewa mkataba rasmi wa miaka mitatu kwa majukumu mapya.
0 comments:
Post a Comment