WENYEJI, Mbeya Kwanza wamelazimishwa sare ya 1-1 na KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Matheo Anthony alianza kuifungia KMC dakika ya pili tu, kabla ya mshambuliaji mwenzake, Habib Kyombo kuisawazishia Mbeya Kwanza dakika ya 90 na ushei.
Kwa sare hiyo, Mbeya Kwanza wanafikisha pointi 12 katika mchezo wa 13 ingawa wanabaki nafasi ya 11 na KMC wanatimiza pointi 15 katika mchezo wa 13 pia na kusogea nafasi ya nane.
0 comments:
Post a Comment