• HABARI MPYA

    Monday, January 24, 2022

    MUKOKO AACHANA NA YANGA, ATUA MAZEMBE


    KIUNGO Tonombe Mukoko ameachana na klabu ya Yanga na kujiunga na TP Mazembe ya kwao, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
    Taarifa ya Yanga jioni hii imemshukuru Mukoko kwa mchango wake kama Nahodha Msaidizi kwa kipindi cha msimu mmoja na nusu tangu awasili kutoka AS Vita ya kwao, Kinshasa.
    Mukoko anakwenda Mazembe wiki moja baada ya Yanga kumsajili Mkongo mwingine, winga Chico Ushindi kutoka klabu hiyo ya Lubumbashi.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MUKOKO AACHANA NA YANGA, ATUA MAZEMBE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top