• HABARI MPYA

    Saturday, January 22, 2022

    AZAM FC YAITANDIKA PRISONS 4-0 SUMBAWANGA


    WENYEJI, Tanzania Prisons wamekiona cha moto baada ya kuchapwa 4-0 na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Nelson Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.
    Mabao ya Azam FC yamefungwa na Tepsi Evance dakika ya 27, Ismail Aziz Kader dakika ya 68, Ibrahim Ajibu dakika ya 70 na Justin Zullu dakika ya 82.
    Azam FC inafikisha pointi 21 na kusogea nafasi ya nne, ikizidiwa pointi moja na Mbeya City baada ya timu zote kucheza mechi 13, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake 11 za mechi 13 na sasa inahamia mkiani.
    Nayo Biashara United imelazimishwa sare ya bila kufungana na Geita Gold Uwanja wa Karume mjini Musoma mkoani Mara.
    Biashara United inafikisha pointi 11 katika mechi ya 13 nafasi ya 14 na Geita Gold sasa ina pointi 14 za mechi 13 pia nafasi ya 10.
    Nao mabingwa watetezi, Simba SC  wametoa sare ya 0-0 na wenyeji, Mtibwa Sugar Uwanja wa Mangunu Complex, Turiani mkoani Morogoro.
    Mtibwa Sugar inafikisha pointi 12 katika mchezo wa 13 na kusogea nafasi ya 13, wakati Simba SC inafikisha pointi 25 katika mchezo wa 12, ingawa inabaki nafasi ya pili, ikizidiwa pointi saba na watani wa jadi, Simba baada ya timu zote kucheza mechi 12.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAITANDIKA PRISONS 4-0 SUMBAWANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top