TIMU ya Kagera Sugar imesajili washambuliaji wawili wapya katika dirisha hili dogo kuimarisha kikosi chake kuelekea sehemu iliyobaki ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Hao ni mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ aliyewika klabu za Yanga na Simba za Dar es Salaam na Freddy Cossmas Lewis aliyewahi kucheza Mwadui FC ya Shinyanga wawili hao wote wakihamia Misenyi, Bukoba Vijijini mkoani Kagera kama wachezaji huru.
0 comments:
Post a Comment