• HABARI MPYA

    Monday, September 11, 2017

    DE BOER ATUPIWA VIRAGO CRYSTAL PALACE

    Frank De Boer amefukuzwa Crystal Palace baada ya matokeo mabaya Ligi Kuu ya England PICHA ZAIDI GONGA HAPA  


    HIZI NDIZO MECHI ZILIZOMFUKUZISHA KAZI DE BOER PALACE

    Agosti 12: v Huddersfield (nyumbani) - lost 3-0
    Agosti 19: v Liverpool (ugenini) - lost 1-0
    Agosti 22: v Ipswich Town (LC) - won 2-1 
    Agosti 26: v Swansea (nyumbani) - lost 2-0
    Sept 10: v Burnley (ugenini) - lost 1-0 
    KOCHA Frank de Boer amefukuzwa katika klabu ya Crystal Palace leo na nafasi yake itachukuliwa na Roy Hodgson Uwanja wa Selhurst Park. 
    De Boer anafukuzwa kutokana na matokeo mabaya, baada ya kushindwa kupata japo pointi au kufunga bao moja katika mechi nne za awali za Ligi Kuu ya England, ikiwemo ya Jumapili ambayo walifungwa na Burnley.
    Hodgson anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili The Eagles baada ya kumzidi kocha mwenzake wa zamani wa England, Hodgson na Sam Allardyce waliyekuwa naye sambamba katika kwenye mbio za kuwania nafasi hiyo. 
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka The 70 anatarajiwa kurejea kwenye Ligi Kuu ya England kwa mara ya kwanza tangu alipoondoka West Brom kujiunga na timu ya taifa mwaka 2012, baada ya awali kuzifundisha Liverpool, Fulham na Blackburn katika michuano hiyo mikubwa ya klabu nchini humo. 
    Amekuwa nje ya kazi tangu England ivurunde kwenye michuano ya Euro 2016, ilipotolewa na Iceland, lakini mtu huyo kutoka taifa la Croydon anakwenda kufundisha klabu aliyoichezea akiwa kijana mdogo miaka ya 1960.
    Kuondoka kwa De Boer pia kutamfanya na Sammy Lee aondoke klabuni hapo, ambaye aliingia kwenye klabu hiyo pamoja na Allardyce, na Ray Lewington anawasili katika benchi la Ufundi la Hodgson.

    WASIFU WA KOCHA HODGSON 

    1976–1980: Halmstad
    1982: Bristol City
    1982: Oddevold
    1983–1984: Orebro
    1985–1989: Malmö
    1990–1992: Neuchâtel Xamax
    1992–1995: Switzerland
    1995–1997: Inter Milan  
    1997–1998: Blackburn Rovers
    1999: Inter Milan (caretaker) 
    1999–2000: Grasshoppers 
    2000–2001: Copenhagen
    2001: Udinese
    2002–2004: United Arab Emirates
    2004–2005: Viking
    2006–2007: Finland
    2007–2010: Fulham
    2010–2011: Liverpool
    2011–2012: West Bromwich Albion
    2012–2016: England 
    2017: Crystal Palace 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DE BOER ATUPIWA VIRAGO CRYSTAL PALACE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top