WAKATI zinatarajiwa kuteremka dimbani Saa 1:00 usiku Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga katika mchezo wa Nusu Fainali ya Ngao ya Jamii, klabu za Simba na Singida Fountain Gate hazitaruhusiwa kutumia wachezaji wake wa kigeni leo.
Taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imesema kwamba Simba na Singida ndio klabu pekee ambazo hazijawasilisha vibali vya wachezaji wake wa kigeni kwa ajii ya michuano ya Ngao ya Jamii iliyoanza jana.
0 comments:
Post a Comment