TIMU ya Mashujaa FC imelazimishwa sare ya bila kufungana na Geita Gold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.
Hiyo ni sare ya kwanza kwa timu zote baada ya kuanza na ushindi katika mechi za kwanza, Mashujaa ikiichapa Kagera Sugar 2-0 hapo hapo Lake Tanganyika na Geita Gold ikiwalaza wenyeji, Ihefu SC huko Mbarali mkoani Mbeya.
0 comments:
Post a Comment