WAKATI Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara inaanza leo, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa orodha ya makocha wanaokidhi vigezo vya kufanya kazi, huku Makocha wasaidizi, Ouanane Sellami wa Simba na Moussa Ndaw wa Yanga wakiwa hawana sifa hizo.
Wengine ni Corneille Hategekimana ambaye ni Kocha wa viungo wa Simba, Melisa Medo wa Dodoma Jiji, Mwinyi Zahera wa Coastal Union, Hans Van Der Pluijm wa Singida Fountain Gate, Yousupho Dabo wa Azam FC, wakati Tabora United na Mtibwa Sugar mabenchi yote kuanzia Kocha mkuu wa wasaidizi wao wote hawana vigezo.
0 comments:
Post a Comment