Mabao ya Azam FC yamefungwa na nyota wake, mshambuliaji wa Kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube Mpumelelo dakika ya kwanza na kiungo chipukizi wa Kimataifa wa Tanzania, Abdul Suleiman Sopu dakika ya 42.
Azam iliangukia kwenye mchezo wa kuwania nafasi ya tatu baada ya kufungwa 2-0 na Yanga kwenye mchezo wa Nusu Fainali Jumatano, wakati Singida Fountain Gate ilitolewa kwa penalti 4-2 na Simba baada sare ya bila kufungana hapo hapo Mkwakwani.
Mchezo wa Fainali ya Ngao ya Jamii utafuatia Saa 1:00 usiku hapo hapo Uwanja wa Mkwakwani baina ya Simba na Yanga.
0 comments:
Post a Comment