WENYEJI, Chelsea wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Liverpool katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Jumapili Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Luis Diaz alianza kuifungia Liverpool inayofundishwa na Kocha Mjerumani, Jurgen Klopp dakika ya 18, kabla ya Axel Disasi kuisawazishia Chelsea ya kocha Muargentina, Mauricio Pochettino dakika ya 37 katika mchezo huo wa kwanza wa msimu kwa timu hizo.
0 comments:
Post a Comment