BONDIA Muingereza mwenye asili ya Nigeria, Anthony Oluwafemi Olaseni Joshua amerejesha heshima baada ya ushindi wa Knockout (KO) raundi ya saba dhidi ya Robert Helenius wa Finland katika pambano la uzito wa juu usiku wa jana ukumbi wa O2 Arena Jijini London, UK.
Baada ya ushindi huo, bingwa huyo wa zamani wa WBA, IBF, WBO na IBO), amesema sasa anataka kuzipiga na Mmarekani, bingwa wa zamani wa WBC, Deontay Leshun Wilder ambaye naye alimpiga Helenius kwa KO raundi ya kwanza tu Oktoba mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment