Shujaa wa Simba kwa mara nyingine leo amekuwa kipa Ally Salum aliyeokoa penalti tatu mfululizo za viungo Mganda Khalid Aucho, Pacome Zouzoua na beki Kouassi Attohoula Yao, wote wa Ivory Coast, huku Mburkinabe Stephane Aziz Ki pekee akifunga upande wa Yanga.
Waliofunga penalti za Simba ni kiungo wa Kimataifa wa Tanzania, Muzamil Yassin na washambuliaji Mcameroon Leandre Willy Essomba Onana na Mkongo, Jean Othos Baleke huku Mrundi Saido Ntibanzokiza iliokolewa na kipa Mmali, Djigui Diarra na ya Mzambia, Moses Phiri ikienda juu ya lango.
Simba ilifika Fainali kwa ushindi wa penalti pia 4-2 dhidi ya Singida Fountain Gate Alhamisi huku Yanga wakiifunga Azam FC 2-0 Jumatano.
0 comments:
Post a Comment