WENYEJI, Chelsea wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Southampton katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Mabao y Chelsea leo yamefungwa na Trevoh Chalobah dakika ya tisa, Timo Werner dakika ya 84 na Ben Chilwell dakika y 89, wakati la Southampton limefungwa na James Ward-Prowse kwa penalti dakika ya 61.
The Blues wanapanda kileleni baada y kufikisha pointi 16 katika mchezo wa saba, mbele ya Liverpool yenye pointi 14 sawa na na Manchester United na Everton zinazofuatia.
0 comments:
Post a Comment