• HABARI MPYA

    Sunday, October 24, 2021

    REAL YAICHAPA BARCA 2-1 CAMP NOU

    WENYEJI, Barcelona wamechapwa mabao 2-1 na mahasimu wao, Real Madrid katika mchezo wa La Liga jioni ya leo Uwanja wa Camp Nou, Barcelona.
    Mabao ya Real Madrid yamefungwa na David Alaba dakika ya 32 akimalizia pasi ya Rodrygo na Lucas Vázquez dakika ya 90 na ushei dakika nne kabla ya 
    Sergio Agüero kuifungia Barca la kufutia machozi katika muda wa ziada.
    Real Madrid inafikisha pointi 20 na kupanda kileleni mwa La Liga ikizizidi wastani wa mabao tu Sevilla na Real Sociedad, wakati Barcelona inabaki na pointi zake 15 katika nafasi ya nane baada ya timu zote kucheza mechi tisa.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REAL YAICHAPA BARCA 2-1 CAMP NOU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top