HATIMAYE Barcelona imepata ushindi wake wa kwanza katika Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuichapa Dynamo Kiev 1-0, bao pekee la mlinzi Gerard Pique katika mchezo wa Kundi E Uwanja wa Camp Nou.
Kwa pointi hizo tatu za kwanza baada ya mechi tatu Barcelona inayofundishwa na kocha Ronald Koeman inapanda nafasi ya tatu, mbele ya Dynamo Kiev yenye pointi moja na nyuma ya Benfica yenye pointi nne na vinara, Bayern Munich wenye pointi tisa.
0 comments:
Post a Comment