RAIS WA Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan jana alizungumza kwa simu na wachezaji wa taifa ya wakubwa ya wanawake, Twiga Stars na ya wasichana chini ya umri miaka 20, Tanzanite na kuahidi kuwafanyia jambo akirejea Dar es Salaam.
Mama Samia alizungumza na wachezaji hao jana kupitia simu ya Katibu wa Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo wakati wa hafla maalum ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na Serikali kuwapongeza wachezaji hao kwa mafanikio yao.
Wakati Twiga Stars ilitwaa ubingwa wa COSAFA Afrika Kusini mwishoni mwa wiki, wadogo zao Tanzanite waliitoa Eritrea katika mbio za kuwania tiketi ya Kombe la Dunia la U20 mwakani Costa Rica.
0 comments:
Post a Comment