• HABARI MPYA

    Wednesday, October 06, 2021

    MANAHODHA WOTE AZAM FC WASIMAMISHWA


    KLABU ya Azam FC imewasimamisha wachezaji wake watatu, beki na Nahodha, Aggrey Morris pamoja na Wasaidizi wake, viungo Salum Abubakar 'Sure Boy' na Mudathir Yahya kwa kile kilichoelezwa makosa ya utovu wa nidhamu.
    Taarifa ya Azam FC iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya klabu hiyo, Thabit Zacharia imesema watatu kwa pamoja walimtolea maneno yasiyofaa Meneja wa timu hiyo, Luckson Kakolaki.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANAHODHA WOTE AZAM FC WASIMAMISHWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top