• HABARI MPYA

    Thursday, October 07, 2021

    TWIGA STARS YATINGA FAINALI COSAFA

     TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la COSAFA baada ya ushindi wa penalti 3-0 kufuatia sare ya 1-1 na Zambia mchana wa leo Uwanja wa Nelson Mandela Bay Jijini Port Elizabeth, Afrika Kusini.
    Shujaa wa Twiga Stars leo alikuwa ni kipa, Janet Simba aliyeokoa mikwaju miwili ya penalti ya Zambia. 
    Finali ni Jumamosi na Twiga Stars itamenyana na Malawi iliyoichapa Afrika Kusini 3-2 jioni ya leo katika Nusu Fainali nyingine hapo hapo Port Elizabeth. Zambia na Afrika Kusini watawania nafasi ya tatu mapema Jumamosi.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TWIGA STARS YATINGA FAINALI COSAFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top