TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars imetupwa nje mbio za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuchapwa 3-2 na Namibia jioni ya leo Uwanja wa Dobsonville Jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Mabao ya Namibia leo yamefungwa na kiungo mshambuliaji wa Sevilla ya Hispania, Zenatha Goeieman Coleman yote matatu, wakati ya Twiga Stars yamefungwa na kiungo mshambuliaji wa Chabab Atlas Khenifra ya Morocco Mwanahamisi Omary Shaluwa ’Gaucho’ na mshambuliaji wa Simba Queens, Opa Clement Sanga. Twiga Stars inatolewa kwa jumla ya mabao 5-3 baada ya kuchapwa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza Jumatano Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Siku hiyo mabao ya Namibia yote yalifungwa na Coleman, wakati bao pekee la Twiga Stars lilifungwa na kiungo wa JKT Queens, Stumai Abdallah Athumani.
Reports: Jack Wilshere set for Arsenal return
-
Former Arsenal midfielder Jack Wilshere has held talks with the north
London side on one of its vacant academy coaching roles. Under 23 manager
Per Mertes...
YANGA ‘KUPAA’ JUMANNE KUIFUATA MWADUI FC
-
MARA baada ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc kwenye uwanja wa
Majaliwa, Lindi, siku ya jumapili, Kikosi cha Young Africans Sports Club,
kitareje...
0 comments:
Post a Comment