• HABARI MPYA

    Saturday, October 16, 2021

    CHELSEA YAREJEA KILELENI ENGLAND


    BAO pekee la beki wa kimataifa wa England, Ben Chilwell dakika ya 45 limeipa Chelsea ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Brentford Uwanja wa Brentford Community, Brentford, Middlesex.
    Kwa ushindi huo kwenye mchezo ambao kipa Msenegal, mzaliwa wa Ufaransa, Edouard Mendy alijizolea sifa kemkem kwa kuokoa michomo mingi, Chelsea inafikisha pointi 19 na kurejea kileleni sasa ikiizidi pointi moja Liverpool baada ya wote kucheza mechi nane.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA YAREJEA KILELENI ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top