TIMU ya Liverpool jana iliichapa Watford mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Anflied.
Mabao ya Liverpool yamefungwa na Diogo Jota dakika ya 22 na Fabinho dakika ya 89 kwa penalti na kwa ushindi huo, Liverpool inafikisha pointi 72, ingawa inabaki na nafasi ya pili ikizidiwa pointi moja na mabingwa watetezi, Manchester City baada ya wote kucheza mechi 30.
0 comments:
Post a Comment