SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limemteua refa Frank Komba wa Tanzania kuwa miongoni mwa waamuzi watakaochezesha mchezo wa Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika, baina ya wenyeji, Mamelodi Sundowns na Petro Atlètico ya Angola Aprili 24, mwaka huu Uwanja wa FNB Jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
Kwa upande wake, Meneja Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto ameteuliwa na CAF kuwa Mratibu (General Coordinator) wa mchezo wa Robo fainali Kombe la Shirikisho Afrika kati ya wenyeji, Al-Masry SC na RS Berkane Ya Morocco Aprili 17, mwaka huu nchini Misri.
0 comments:
Post a Comment