• HABARI MPYA

    Saturday, April 23, 2022

    GEITA GOLD YAILAMBA KMC 2-0 NYANKUMBU


    WENYEJI, Geita Gold wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Nyankumbu mjini Geita.
    Mabao ya Geita Gold ya kocha Freddy Felix Minziro yamefungwa na Amos Charles dakika ya 48 na George Mpole dakika ya 75 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 27 katika mchezo wa 20 na kupanda nafasi ya tano, ikizidiwa pointi moja na Azam FC ambayo hata hivyo ina mechi moja mkononi.
    KMC baada ya kichapo cha leo inabaki na pointi zake 24 za mechi 21 ikishukia nafasi ya tisa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GEITA GOLD YAILAMBA KMC 2-0 NYANKUMBU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top