• HABARI MPYA

    Saturday, April 23, 2022

    ARSENAL YAICHAPA MAN UNITED 3-1 EMIRATES


    WENYEJI, Arsenal wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Emirates Jijini London.
    Mabao ya Arsenal yamefungwa na Nuno Tavares dakika ya tatu, Bukayo Saka dakika ya 32 kwa penalti na Granit Xhaka dakika ya 70, wakati la Man United limefungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya 34 huku Bruno Fernandes akikosa penalti dakika ya 57.
    Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 60 katika mchezo wa 33 na kujiweka sawa nafasi ya nne, ikiizidi pointi sita Man United ambayo imecheza mechi moja zaidi na inabaki nafasi ya sita.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YAICHAPA MAN UNITED 3-1 EMIRATES Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top