BEKI wa Orlando Pirates, Fortune Makaringe akimuangusha winga Mghana wa Simba, Bernard Morrison kwenye boksi jana katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika jana Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Refa Mtunisia, Haythem Guirat aliamuru mkwaju wa penalti ambao uliwekwa nyavuni na beki kimataifa wa Tanzania, Shimari Salum Kapombe kuipatia bao pekee Simba katika mchezo huo.
Timu hizo zitarudiana Jumapili ijayo Uwanja wa Orlando Pirates Jijini Johannesburg na mshindi wa jumla atakwenda Nusu Fainali.
0 comments:
Post a Comment