SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limekubali ombi la klabu ya Simba kuongoza mashabiki 60,000 katika mchezo wake wa kwanza wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini.
Aidha, katika mchezo huo utakaofanyika Jumapili ya Aprili 17, mwaka huu kuanzia Saa 1:00 usiku Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, CAF pia imesema utakuwa teknolojia ya VAR itatumika kwa mara ya kwanza Tanzania.
0 comments:
Post a Comment