• HABARI MPYA

    Saturday, April 16, 2022

    POLISI YATOA SARE TENA MOSHI, 1-1 NA MBEYA KWANZA


    WENYEJI, Polisi Tanzania wamelazimishwa sare ya 1-1 na Mbeya Kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
    Habib Kyombo alianza kuifungia Mbeya Kwanza dakika ya 23, kabla ya Kassim Shaaban kuisawazishia Polisi dakika ya 34.
    Kwa matokeo hayo, Polisi inafikisha pointi 25 na kusogea nafasi ya sita, wakati Mbeya Kwanza inafikisha pointi 15, ingawa inaendelea kuzibeba timu nyingine zote 15 kwenye msimamo wa Ligi baada ya wote kucheza mechi 20.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: POLISI YATOA SARE TENA MOSHI, 1-1 NA MBEYA KWANZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top