• HABARI MPYA

    Thursday, April 21, 2022

    ARSENAL YAIPIGA CHELSEA 4-2 PALE PALE DARAJAN


    TIMU ya Arsenal imeibuka na ushindi wa 4-2 dhidi ya wenyeji, Chelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Jumatano Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
    Mabao ya Arsenal yamefungwa na Eddie Nketiah dakika ya 13 na 57, Emile Smith Rowe dakika ya 27 na Bukayo Saka  dakika ya 90 na ushei kwa penalti, wakati ya Chelsea yamefungwa na Timo Werner dakika ya 17 na Nahodha wake, Cesar Azpilicueta dakika ya 32.
    Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 57 katika mchezo wa 32 na kurejea nafasi ya tano, wakati Chelsea inabaki na pointi zake 62 za mechi 31 nafasi ya tatu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YAIPIGA CHELSEA 4-2 PALE PALE DARAJAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top