TIMU ya Real Madrid imetanguliza mguu moja Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya wenyeji, Chelsea kwenye mchezo wa kwanza wa Robo Fainali usiku huu Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Mabao yote ya Real Madrid yamefungwa na mshambuliaji Mfaransa, Karim Benzema dakika ya 21, 24 na 46, wakati la Chelsea limefungwa na Kai Havertz dakika ya 40.
0 comments:
Post a Comment