MABINGWA watetezi, Simba SC wamelazimishwa sare ya bila mabao na wenyeji, Polisi Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Chuo cha Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Kwa sare hiyo inayoiongezea kila timu pointi moja, Simba inafikisha pointi 41 na wanabaki nafasi ya pili, wakizidiwa pointi 10 na watani wao wa jadi, Yanga SC baada ya wote kucheza mechi 19.
Polisi Tanzania inafikisha pointi 24 katika mchezo wa 19 pia na kusogea kwa nafasi moja hadi ya nane.
0 comments:
Post a Comment