• HABARI MPYA

    Sunday, April 03, 2022

    BRENTFORD YAITANDIKA CHELSEA 4-1 STAMFORD BRIDGE


    TIMU ya Brentford jana ilitoka nyuma na kushinda 4-1 dhidi ya wenyeji, Chelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
    Chelsea ilitangulia kwa bao la Antonio Rudiger dakika ya 
    48, kabla ya Brentford kuzinduka kwa mabao ya Vitaly Janelt dakika ya 50 na 60, Christian Eriksen dakika ya 54 na Yoane Wissa dakika ya 87.
    Ushindi huo unaifanya Brentford ifikishe pointi 33 katika mchezo wa 31 na kujivuta nafasi ya 14, wakati Chelsea inabaki na pointi zake 59 za mechi 29 katika nafasi ya tatu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BRENTFORD YAITANDIKA CHELSEA 4-1 STAMFORD BRIDGE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top