BAO la George Mpole Mwaigomole dakika ya 14, limewapa Geita Gold ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Kwa ushindi huo, Mpole akiiadhibu timu yake ya zamani, Geita Gold inafikisha pointi 24 na kupanda nafasi ya sita, wakati Mbeya City inabaki na pointi zake 25 katika nafasi ya tano baada ya timu zote kucheza mechi 19.
0 comments:
Post a Comment