MOURINHO ATUNGULIWA PENALTI ZOTE MECHI YA HISANI ENGLAND
Kipa wa Team Shearer, Jose Mourinho akiruka kuokoa bila mafanikio moja ya mikwaju ya penalti katika mchezo wa kirafiki wa Hisani dhidi ya Team Ferdinandi leo Uwanja wa Loftus Road leo maalum kuchangisha fedha za kuwasaidia wahanga wa ajali ya moto ya Grenfell Juni mwaka huu. Team Ferdinand imeshinda kwa penalti 5-3 baada ya sare ya 2-2 maana yake Mournho alishindwa kuokoa hata mkwaju mmoja. Mabao ya Team Ferdinand yamefungwa na mwanariadha bingwa wa Olimpiki, Mo Farah na Chris Edwards wakati ya Team Shearer yamefungwa na Trevor SinclairPICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment