• HABARI MPYA

    Wednesday, November 22, 2023

    KAGERA SUGAR YAAMBULIA SARE TU KWA KMC 1-1 KAITABA


    WENYEJI, Kagera Sugar wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
    Kagera Sugar walitangulia na bao la beki wake Mganda, Deus Bukenya dakika ya 49, kabla ya mshambuliaji Waziri Junior Shentembo kuisawazishia KMC dakika ya 74.
    Kwa matokeo hayo, KMC inafikisha pointi 16 na kupanda nafasi ya nne, wakati Kagera Sugar sasa ina jumla ya pointi 13 na inasogea nafasi ya saba baada ya wote kucheza mechi 10.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAGERA SUGAR YAAMBULIA SARE TU KWA KMC 1-1 KAITABA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top