• HABARI MPYA

    Saturday, November 04, 2023

    MANCHESTER CITY YAIFUMUA BOURNEMOUTH 6-1 ETIHAD


    MABINGWA watetezi, Manchester City wamerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya England baada ya ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya AFC Bournemouth leo Uwanja wa Etihad Jijini Manchester.
    Mabao ya Manchester City yamefungwa na Jeremy Doku dakika ya 30, Bernardo Silva mawili, dakika ya 33 na 83, Manuel Akanji dakika ya 37, Philip Foden dakika ya 64, Phil Foden dakika ya 64 na Nathan Ake  dakika ya 88, wakati bao pekee la Bournemouth limefungwa na Luis Sinisterra dakika ya 74.
    Kwa ushindi huo, Manchester City inafikisha pointi 27 katika mchezo wa 11 na kurejea kileleni, ikiizidi pointi moja Tottenham Hotspur ambayo pia ina mchezo mmoja mkononi, wakati Bournemouth inabaki na pointi zake sita za mechi 12 pia nafasi ya 17.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANCHESTER CITY YAIFUMUA BOURNEMOUTH 6-1 ETIHAD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top