MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa Burkina Faso, Stephane Aziz Ki ameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Yanga SC kwa mwezi Oktoba akiwaangusha beki mzawa, Dickson Job na kiungo Mkongo, Maxi Mpia Nzengeli.
Kwa ushindi huo, Aziz Ki aliyefunga mabao yote matatu katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Azam FC Oktoba 23 atazawadiwa kitita cha Sh. Milioni 4 kutoka kwa wadhamini, Shirika la Bima la Taifa (NIC).
0 comments:
Post a Comment