WENYEJI, Coastal Unión wameibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Geita Gold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga. Geita Gold ilitangulia kwa bao la Valentino Mashaka dakika ya 12, kabla ya Coastal Unión kutoka nyuma kwa mabao ya kiungo Mbenin, Roland Junior Beakou dakika ya 30, Maabad Maulid dakika ya 53 na Charles Semfuko dakika ya 59. Kwa ushindi huo, Coastal Unión inafikisha pointi 13 na kusogea nafasi ya tisa, sawa na Geita Gold inayoshukia nafasi ya 10 baada ya wote kucheza mechi 12.
Reports: Jack Wilshere set for Arsenal return
-
Former Arsenal midfielder Jack Wilshere has held talks with the north
London side on one of its vacant academy coaching roles. Under 23 manager
Per Mertes...
YANGA ‘KUPAA’ JUMANNE KUIFUATA MWADUI FC
-
MARA baada ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc kwenye uwanja wa
Majaliwa, Lindi, siku ya jumapili, Kikosi cha Young Africans Sports Club,
kitareje...
0 comments:
Post a Comment