KOCHA wa Arsenal, Mikel Arteta jana alikuwa mwenye furaha baada ya timu yake kuweka kando machungu ya kichapo cha 1-0 kutoka Newcastle United Jumamosi katika Ligi Kuu ya England na kuilaza Sevilla 2-0.
Mabao ya Arsenal jana yamefungwa Leandro Trossard dakika ya 29 na Bukayo Saka dakika ya 64 Uwanja wa Emirates Jijini London kwenye mchezo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Matokeo hayo yanaiweka Arsenal kileleni mwa Kundi B ikiwa na pointi tisa, ikifuatiwa naPSV na Lens zenye pointi tano kila moja, wakati Sevilla inaendelea kushika mkiani baada ya wote kucheza mechi nne.
0 comments:
Post a Comment