• HABARI MPYA

    Sunday, November 26, 2023

    GARNACHO APIGA BONGE LA BAO MAN UNITED YASHINDA 3-0 LIVERPOOL


    TIMU ya Manchester United imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji, Everton katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Goodison Park Jijini Liverpool.
    Mabao ya Manchester United leo yamefungwa na washambuliaji Mspaniola Alejandro Garnacho dakika ya tatu, Muingereza Marcus Rashford kwa penalti dakika ya 56 na Mfaransa, Anthony Martial dakika ya 75.
    Kwa ushindi huo, Manchester United inafikisha pointi 24 na kusogea nafasi ya sita, wakati Everton inabaki na pointi zake nne nafasi ya 19 baada ya wote kucheza mechi 13.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GARNACHO APIGA BONGE LA BAO MAN UNITED YASHINDA 3-0 LIVERPOOL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top