• HABARI MPYA

    Thursday, November 23, 2023

    TANZANIA PRISONS YATAMBULISHA KOCHA MBADALA WA MINZIRO


    KLABU ya Tanzania Prisons imemtambulisha Hamad Hamisi Ally kuwa kocha wake mpya Mkuu, ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili kufundisha timu hiyo katika Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara.
    “Tumefanikiwa kuingia mkataba wa miaka miwili (2) na Kocha Hamad Hamisi Ally. Kocha Hamad anakuja kuwa kocha mkuu wa timu yetu kuanzia hii leo na uongozi unaimani kubwa juu yake,” imesema taarifa ya Tanzania Prisons leo.
    Uongozi wa Tanzania Prisons chini ya Mtendaji Mkuu, Ajabu Adam Kifukwe umemtakia kila la kheri kocha Hamad katika majukumu yake yake mapya.
    Hamad anachukua nafasi ya Freddy Felix Minziro aliyeondolewa mapema wiki hii kutokana na mwenendo mbaya wa timu katika Ligi Kuu ikiambulia pointi saba katika mechi tisa za awali, hivyo kujikuta nafasi ya 14 kwenye Ligi ya timu 16, ambayo mwisho wa msimu mbili zitashuka na mbili zitakwenda kwenye mchujo wa kuwania kubaki.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA PRISONS YATAMBULISHA KOCHA MBADALA WA MINZIRO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top