• HABARI MPYA

    Friday, July 21, 2023

    MISS TANZANIA 2023 KUONDOKA NA BENZ NA SH MILIONI 10 LEO MASAKI


    WAREMBO 20 wabaki vinywa wazi mara baada ya kutangazwa rasmi zawadi ya Miss Tanzania   gari aina ya Mercedes benz yenye thamani ya Shilingi Milioni 30 za Kitanzania pamoja na pesa taslim  Milioni 10 kwa atakaeibuka Mshindi Usiku wa Leo  katika ukumbi wa Superdome Masaki Jijini Dar es salaam. 
    Akizungumza na Wanahabari wakati wa kutambulisha zawadi hiyo. Jijini Dar es salaam Meneja Masoko wa Kampuni ya Startimes David Malisa, amesema kuwa Fainali ya Miss Tanzania  itapambwa na burudani mbalimbali kutoka kwa warembo wenyewe huku akisisitiza kuwa Fainali hiyo itakuwa ya kitofauti kutokana na kupangika kwa matukio ya kiburudani zaidi.
    "Nilipata nafasi ya kupita kambini kushuhudia mazoezi ya Fainali ya Miss Tanzania kutoka kwa washiriki wenyewe Kiukweli kuna hatari watu wanajifua namna ya kutembea jukwaani (catwalk) zaidi ya Mrembo Halima Kopwe (Miss Tanzania 2021) lipieni ving'amuzi mshuhudie burudani hiyo kupitia chaneli ya  St bongo ndani ya Startimes. "
    Malisa amewasihi watazamaji kulipia mapema ving'amuzi vyao ili kutazama mubashara Fainali hizo kwa wale ambao hawatabahatika kufika katika ukumbi wa the Superdome Masaki Jijini Dar es salaam. 
     Nae Meneja Mradi wa shindano hilo Ombeni Phiri amesema Washiriki hao  20 kutoka  kanda mbalimbali wanaenda kugombania gari hiyo ambapo ni kwa mara ya pili mfululizo gari aina ya Mercedes benz kutolewa kwa mshindi.
    "Warembo 20 wamekuwa kambi kwa siku 27 na kujifunza vitu mbalimbali hivyo sio jambo rahisi kwa warembo hao  kuwa sehemu moja kutokana na kila mshiriki ana tabia yake.''
    Hata hivyo Phiri amewatakia kila la heri warembo hao 20 kuelekea fainali hiyo ambapo mmojawapo anaenda kubadilisha maisha yake kupitia tasnia ya urembo na mitindo. 

    Hata hivyo kwa upande Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Azam Mashango amesema washiriki wote 20 watapewa fedha kama kiinua mgongo isipokuwa  Mshindi wa nne,tano na sita  watapewa Milioni 1 ,Mshindi wa 3 milioni 2 huku Mshindi wa pili akipatiwa Milioni 2 na wa kwanza milioni 10 huku Mshindi wa 6 hadi 20 wakiambulia laki 2 kila mmoja. 
    Mashango amewapongeza wadau mbalimbali wa shindano hilo wakiwemo Robby One pharmacy, Startimes na wengine  kuhakikisha shindano hilo linafanyika na linaonyeshwa mubashara kwenye King'amuzi hicho ili kuwapa nafasi wadau wa urembo kuwaona wasichana hao wadogo wenye kiu ya kutimiza ndoto zao kupitia tasnia ya urembo. 
    ORODHA YA WASHINDI WA TAJI LA MISS TANZANIA
    2023 Halima Kopwe
    2022 Juliana Rugumisa
    2019 Sylvia Sebastian
    2018 Queen Elizabeth Makune
    2017 Julitha Kabete
    2016 Diana Edward Lukumay
    2015 Lilian Kamazima
    2014 Happiness Watimanywa
    2013 Brigitte Alfred Lyimo
    2012 Lisa Jensen
    2011 Salha Kifai
    2010 Genevieve Emmanuel Mpangala
    2009 Miriam Gerald Unplaced
    2008 Nasreen Karim
    2007 Richa Adhia
    2006 Wema Sepetu
    2005 Nancy Sumari
    2004 Faraja Kotta
    2003 Sylvia Bahame
    2002 Angela Damas
    2001 Happiness Magese
    2000 Jacqueline Ntuyabaliwe
    1999 Hoyce Temu
    1998 Basila Mwanukuzi
    1997 Saida Kessy
    1996 Shose Sinare
    1995 Emily Adolf
    1994 Aina Maeda
    1967 Theresa Shayo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MISS TANZANIA 2023 KUONDOKA NA BENZ NA SH MILIONI 10 LEO MASAKI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top