ALIYEKUWA kocha wa Yanga, Nasredeen Nabi amejiunga na na mabingwa wa Morocco, FAR Rabat kwa mkataba wa miaka miwili na ataanza kazi mara moja.
Nasredeen Nabi, raia wa Tunisia aliachana na Yanga baada ya msimu mzuri akiipa mataji yote ya nyumbani, Ngao ya Jamii, ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) pamoja na kuifikisha Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
0 comments:
Post a Comment