KLABU ya Simba SC imetoa sare ya kufungana bao 1-1 na Zira FK ya Azerbaijan katika mchezo wake wa kwanza wa kujipima kwenye kambi yake ya kujiandaa na msimu mpya mjini Ankara nchini Uturuki.
Bao la Simba SC inayofundishwa na Kocha Mbrazil, Robert Oliveira ‘Robertinho’ limefungwa na kiungo mshambuliaji, Kibu Dennis Prosper dakika ya 33 huku la Zira FK limefungwa na kiungo Rustam Alamovych Akhmedzade anayecheza kwa mkopo kutoka Qarabağ dakika ya 63.
0 comments:
Post a Comment